Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 06:07

Majeshi ya Niger na Burkina Faso yasema yameua magaidi 100 katika operesheni ya pamoja


Ramani ya Niger
Ramani ya Niger

Wakuu wa jeshi la Niger na jeshi la Burkina Faso Jumatatu wamesema operesheni ya pamoja ya wiki tatu katika eneo la mpakani linaloshambuliwa sana na wanajihadi, iliua magaidi 100 na wanajeshi wawili kupoteza maisha.

Operesheni hiyo iliyopewa jina la Taanli 3 iliendeshwa kati ya tarehe 2 na 25 Aprili ilifanikishwa na ndege za upelelezi na kivita, wakuu wa majeshi ya nchi hizo mbili wamesema katika ripoti.

Wamesema operesheni hiyo “iliua takriban magaidi 100,” 40 walikamatwa, iliharibu ngome 40 za wanajihadi na kupokonya vifaa vyao.

Wameongeza kuwa wanajeshi wawili walifariki na wengine wawili kujeruhiwa, bila kutaja uraia wao.

Niger na Burkina Faso zimekuwa zikishambuliwa na uasi wa kijihadi ulioanzishwa kutoka nchi jirani ya Mali mwaka 2015.

Maelfu ya watu waliuawa na maelfu ya wengine walitoroka makazi yao kutokana na uasi huo.

XS
SM
MD
LG