Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Januari 24, 2025 Local time: 00:30

Mahathir aapishwa Waziri Mkuu mpya Malaysia


Waziri Mkuu aliyeshindwa uchaguzi Malaysia Najib Razak kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari Kuala Lumpur, Malaysia, Alhamisi, Mei 10, 2018.
Waziri Mkuu aliyeshindwa uchaguzi Malaysia Najib Razak kabla ya kuzungumza na waandishi wa habari Kuala Lumpur, Malaysia, Alhamisi, Mei 10, 2018.

Kiongozi wa zamani wa Malaysia, Mahathir Mohamad(92), ameapishwa Alhamisi kuwa Waziri Mkuu wa saba wa nchi hiyo baada kuushitua ulimwengu kwa kuibuka mshindi wa uchaguzi wa bunge pamoja na kuwa alistaafu muda mrefu.


Waziri Mkuu huyo wa zamani anayejulikana kwa utawala wake wa mabavu, na muungano wa vyama vya upinzani, Alliance of Hope, umekiondoa madarakani muungano wa chama cha Waziri Mkuu Najib Razak, Barisan National Coalition, kilichokuwa kimetawala Malaysia tangia nchi hiyo ipate uhuru mwaka 1957.

Kuchaguliwa kwake kunamfanya kuwa ni kiongozi mkongwe kuliko wote duniani.

Sherehe ya kuapishwa kwake imefanyika ikulu ya Kuala Lumpur na kumaliza uvumi uliokuwa unaenezwa kuwa chama cha Barisan National Coalition kingejaribu kunang'ania madarakani.

Mahathir, aliyekuwa amevalia vazi la utamaduni wa Malaysia na kofia ya Kiislam, aliapishwa na Mfalme Sultan Muhammad katika tafrija iliyofuata utamaduni wa nchi hiyo

Waziri Mkuu Najib Razak alikubali kushindwa Alhamisi, akisema yeye na wenzake katika chama "wamekubali uamuzi wa wananchi."

XS
SM
MD
LG