Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 14:20

Mahakama yakataa maombi ya Trump


Jaji wa mahakama ya shirikisho, Jumatano amekataa maombi ya rais wa zamani wa Marekani, Donald Trump,  ya kusikilizwa upya kwa kesi iliyofunguliwa na E Jean Carroll.

Katika kesi hiyo baraza la mahakama limemkuta rais huyo na makosa ya udhalilishaji wa kijinsia, na kumkashifu mwandishi na kumtaka alipe fidia ya dola za kimarekani milioni 5.

Katika uamuzi wenye kurasa 59, jaji wa mahakama ya wilaya ya Marekani, Lewis Kaplan, mjini Manhattan, amesema baraza la mahakama halikufikia kutoa matokeo makali, na kwamba uamuzi wa Mei 9 haukuwa chini ya kiwango cha haki.

Carroll alimshutumu Trump, kuwa alimbaka katik chumba cha kubadilishia nguo katika duka moja la Manhattan katika miaka ya 1990, na baadaye kuzungumzia tukio hilo katika mtandao wa kijamii wa Trump, unoitwa Truth, kuwa ni uwongo wa kupandikiza hapo Oktoba 22.

Trump anadai kulipa fidia ya dola milioni 2 kwa udhalilishaji wa kijinsia ni fedha nyingi.

Forum

XS
SM
MD
LG