Dwight Sagaray, ambaye alikuwa katibu kiongozi katika ubalozi huo, alikutwa na hatia ya mauaji ya Olga Fonseca Julai 2012, Jaji Roselyn Korir alisema katika uamuzi wake.
Mahakama pia iliwatia hatiani raia watatu wa Kenya waliokuwa wameshtakiwa pamoja na Sagaray, ikisema walihusika katika mpango wa pamoja wa kutekeleza mauaji hayo.
Mshukiwa mwingine aliyekimbia baada ya mauaji hayo bado yuko huru na mahakama ilisema hati yake ya kukamatwa iendelee kutumika.
Sagaray, ambaye alivalia suti na tai kizimbani, alifunika uso wake wakati hukumu hiyo iliposomwa.
Facebook Forum