Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 03:23

Maelfu ya Wapalestina wafanya ibada kwa ajili ya waliopata ajali baharini


Muombolezaji akipokea jeneza la Mpalestina Abdul-Al Omar Abdul-Al ambaye alikuwa kwenye boti iliyokuwa imebeba wahamiaji kutoka Lebanon iliyozama kwenye maji ya Syria, wakiwa katika kambi ya wakimbizi ya Palestina Jumamosi, Septemba 24, 2022.(AP/Bilal Hussein)
Muombolezaji akipokea jeneza la Mpalestina Abdul-Al Omar Abdul-Al ambaye alikuwa kwenye boti iliyokuwa imebeba wahamiaji kutoka Lebanon iliyozama kwenye maji ya Syria, wakiwa katika kambi ya wakimbizi ya Palestina Jumamosi, Septemba 24, 2022.(AP/Bilal Hussein)

Maelfu ya Wapalestina wamefanya ibada  katika uwanja mdogo wa kandanda katika kambi ya wakimbizi kaskazini mwa Lebanon kwa ajili ya ajali mbaya ya baharini kuwahi kutokea katika muda mrefu ambapo wahamiaji wengi walipoteza maisha wiki hii wakati boti yao ilipozama katika pwani ya Syria

Mazishi ya Jumamosi yalifanyika huku idadi ya vifo kutokana na ajali hiyo ya boti ya wahamiaji ikiongezeka na kufikia 89 na kuifanya kuwa mbaya zaidi kufikia sasa huku idadi kubwa ya watu wakikimbia Lebanon inayokumbwa na mzozo wa kiuchumi.

Jeshi la Lebanon lilitangaza kuwa wanajeshi wamemkamata mtu mmoja anayedaiwa kuandaa safari hiyo iliyouwa watu. Mzozo wa kiuchumi wa miaka mitatu wa Lebanon unachukuliwa kuwa mbaya zaidi kuwahi kushuhudiwa duniani tangu miaka ya 1850 na kusababisha robo tatu ya nchi hiyo kuwa maskini.

XS
SM
MD
LG