Macron, akizungumza katika mji mkuu wa Cameroon Yaounde, amesema anataka wanahistoria kutoka nchi hizo mbili kushirikiana kwa kuchunguza yaliyotokea miaka ya nyuma na kubaini “wahusika”.
Viongozi wa kikoloni wa Ufaransa waliwakandamiza kikatili watetezi wa uhuru wa Cameroon waliokuwa na silaha kabla ya uhuru wa nchi hiyo mwaka wa 1960.
Maelfu ya wafuasi wa chama cha Union of the Peoples of Cameroon (UPC), akiwemo kiongozi wa uhuru Ruben Um Nyobe, waliuawa na jeshi la Ufaransa.