Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Julai 13, 2025 Local time: 10:59

Maandamano ya kupinga sheria ya kuongeza umri wa kustaafu yavuruga shughuli karibu na uwanja wa ndege wa Paris


Wasafiri watembea kwa miguu wakiwa na mizigo yao kufuatia mgomo wa wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa Roissy-Charles de Gaulle mjini Paris, Machi 23, 2023
Wasafiri watembea kwa miguu wakiwa na mizigo yao kufuatia mgomo wa wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa Roissy-Charles de Gaulle mjini Paris, Machi 23, 2023

Wafanyakazi wa Ufaransa waliokasirishwa na kuongezwa kwa umri wa kustaafu Alhamisi walifunga njia ya kufika kwenye uwanja wa ndege wa Roissy-Charles de Gaulle mjini Paris kama sehemu ya siku ya maandamano ya kitaifa, na kuwalazimisha baadhi ya wasafiri kufika kwenye uwanja huo kwa miguu.

Huduma za treni zilisitishwa na baadhi ya shule kufungwa huku taka zikiwa zimerundikana mitaani, umeme ulikatwa huku vyama vya wafanyakazi vikiongeza shinikizo kwa serikali kuondoa sheria inayoongeza umri wa kustaafu kwa miaka miwili hadi miaka 64.

Moshi mwingi ulitanda hewani kutoka kwenye rundo la uchafu uliochomwa na kuzuia usafiri kwenye barabara kuu karibu na mji wa Toulouse, kaskazini magharibi mwa Ufaransa.

Msemaji wa mamlaka ya viwanja vya ndege mjini Paris amesema maandamano karibu na mlango wa kuingia kwenye uwanja wa huo wa Roissy hayataathiri safari za ndege.

Maandamano mengine yamepangwa kufanyika nchini kote baadaye mchana, huku maandamano mengine yakilenga pia ghala ya mafuta.

Rais Emmanuel Macron jana Jumatano alisema sheria hiyo ambayo serikali yake iliyopitisha wiki iliyopita bila kura ya bunge, itaanza kutekelezwa mwishoni mwa mwaka huu licha ya hasira kuongezeka nchini kote.

XS
SM
MD
LG