Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Juni 18, 2025 Local time: 03:14

Maambukizi ya Covid-19 yaanza kupanda tena


Mkuu wa WHO Tedros Adhanom
Mkuu wa WHO Tedros Adhanom

Mkuu wa shirika la afya duniani Tedros Adhanom Ghebreyesus wakati akiwa kwenye mkutano wa kimataifa wa kibiashara nchini Thailand amesema kwamba viwango vya maambukizi kutokana na virusi vya corona vimeanza kuongezeka kwenye baadhi ya mataifa yaliyoondoa masharti ya kuzuia maambukizi.

Tedros ameongeza kwamba ni wakati kwa ulimwengu kutadhmini ulichojifunza kutokana na janga hilo. Tedros ameomba mataifa yote yanayotengeneza chanjo yashirikiane na Umoja wa Mataifa katika kuimarisha uzalishaji pamoja na taarifa za kiteknolojia.

Kiongozi huyo ameongeza kusema kwamba ingawa baadhi ya mataifa yameondoa kanuni zilizowekwa, janga hilo bado halijamalizika. Chuo kikuu cha John’s Hopkins kinachofuatilia janga hilo kote ulimwenguni kimesema Ijumaa kwamba kufikia sasa kuna zaidi ya kesi milioni 465 za maambukizi kote ulimwenguni ,pamoja na zaidi ya vifo milioni 6 tangu kuzuka kwa janga hilo mwishoni mwa 2019.

XS
SM
MD
LG