Upimaji unaendelea katika wilaya 11 baada ya shughuli hiyo kuzinduliwa katika wilaya ya Chaoyang, Jumatatu.
Wakaazi wa Beijing wamesema kwamba wanaunga mkono hatu ahiyo ya serikali ili kudhibithi maambukizi ya virusi vya Corona.
Maafisa wamewasihi wakaazi katika baadhi ya sehemu za Beijing kufanyia kazi nyumbani. Baadhi ya sehemu za wazi kama zile za kufanyia mazoezi zimeanza kufungwa.
Visa 70 vya maambukizi ya virusi vya Corona vimeripotiwa tangu wiki iliyopita, ikiwemo visa 33 vilivyoripotiwa hiii leo.
Vifo vya watu 51 kati ya visa 10,000 vya maambukizi ya virusi vya Corona vimeripotiwa katika mji wa Shanghai wenye jumla ya watu milioni 26, ambao shughuli za kawaida zimefungwa.