Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Mei 22, 2025 Local time: 13:33

Maafisa wa ngazi ya juu wa Islamic state wameuawa katika shambulizi la Marekani Syria


Afrisa wa jeshi la Syria akiwa katika makabiliano la wapiganaji wa kundi la Islamic state mjini Hasaka, Syria, January 22, 2022
Afrisa wa jeshi la Syria akiwa katika makabiliano la wapiganaji wa kundi la Islamic state mjini Hasaka, Syria, January 22, 2022

Watu wawili wa kundi la kigaidi la Islamic State wameuawa katika shambulizi lililotekelezwa na wanajeshi wa Marekani mashariki mwa Syria.

Taarifa ya kamandi kuu ya jeshi la Marekani CENTCOM, bila kutoa maelezo zaidi, imesema kwamba jeshi la Marekani limetekeleza operesheni iliyofanikiwa kwa kutumia helikopta mashariki mwa Syria saa nane dakika 57 usiku na kuwaua maafisa wawili wa ISIS.

Kati ya waliouawa ni Anas ambaye ni afisa wa Islamic state katika mkoa wa Syria, aliyesimamia operesheni za kundi hilo mashariki mwa Syria.

Kundi la haki za binadamu linalofuatilia vita vya Syria, limesema kwamba operesheni hiyo ndiyo kubwa zaidi kufanyika Syria katika muda wa wiki tatu zilizopita.

Mkuu wa kundi hilo la kufuatilia vita vya Syria Rai Abdel Rahman, amesema kwamba kitengo cha kupambana na ugaidi cha jeshi la Kikurdi la Syria, kimeshiriki katika operesheni hiyo katika Kijiji cha Al-Zor mashariki mwa mkoa wa Deir el-Zour.

XS
SM
MD
LG