Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 20:00

Watetezi wasema mkutano uliingiliwa bila ya sheria Tanzania


Raia wa Uganda ambaye alihojiwa na vyombo vya habari akisema kuwa anahofia usalama wake kutokana na kuwa ni shoga alipokuwa Nairobi, Kenya, Aug. 7, 2014.
Raia wa Uganda ambaye alihojiwa na vyombo vya habari akisema kuwa anahofia usalama wake kutokana na kuwa ni shoga alipokuwa Nairobi, Kenya, Aug. 7, 2014.

Mawakili wa utetezi wa haki za binadamu (LHR) wenye makao yao makuu Afrika Kusini, wameshtushwa na kitendo cha kukamatwa kwa wanaharakati wa haki za binadamu 13 wakiwemo raia wawili wa Afrika Kusini, nchini Tanzania.

Sanja Bornman wa LHR- Progamu ya Usawa wa Kijinsia amesema, “ Hakuna msingi wa sheria yoyote uliotumika katika kuwakamata watu hawa, na pia kuwapa dhamana na baadae kuifuta.

Ameongeza, "Hili linaonyesha ni jaribio la kuwadhibiti na kuwatishia watu na mawakili wanaotetea haki za binadamu, ambao kisheria walikuwa wanapata maelekezo kutoka kwa wateja wao kwa ajili ya kuchukua hatua za kisheria."

"Jambo hili halikubaliki na ni kinyume na majukumu ya kulinda haki za kibinadamu katika nchi ya Tanzania na kimataifa. Hivyo tunataka vyombo vya serikali kuwaachia huru wale wote waliokamatwa wakiwemo wanaharakati wenzetu wa Afrika Kusini," amesisitiza Bornman.

Polisi nchini Tanzania wanadaiwa kuwa waliingilia kati mkutano wa ushauri wa kisheria uliokuwa unafanyika kuanzisha mkakati wa mchakato wa kisheria Afrika (Isla) na huduma za afya ya jamii na uhamasishaji, huko katika jiji la Dar es Salaam.

Watu hao waliokamatwa mwanzoni waliachiwa kwa dhamana lakini baadae dhamana hiyo ilifutwa. Leo Jumatatu ombi la dhamana yao litapelekwa upya.

Taarifa ya LHR inasema kuwa kukamatwa kwa watu hao kunadaiwa kuwa kulisababishwa na ukweli wa kuwa wanaharakati hao walikuwa “wakihamasisha ushoga.”

Lakini LHR wanaamini kuwa sababu hizi ni dhaifu, na siyo za kweli kutokana na polisi wa Tanzania walikuwa wanashikilia agenda na maandiko ya mkutano huo.

Nyaraka walizonazo polisi zinaonyesha wazi kuwa mkutano huo ulioitishwa na Isla, ulikuwa na lengo la kuchukua maelekezo ya kisheria kwa kinachowezekana katika kukabiliana na changamoto za katazo la serikali katika kufunga vituo ambavyo vinawahudumia watu hasa ambao wanakabiliwa na hatari za Ukimwi.

Polisi pia waliwakamata watu 20 kati yao wanane ni wanaume na 12 wanawake kwa makosa ya ushoga katika kisiwa cha Zanzibar mwezi uliopita.

Mwezi Februari, Tanzania ilikosolewa na Marekani baada ya kutangaza kufunga vituo vya afya kadhaa vinavyoshughulikia kuelimisha watu kujilinda na Ukimwi, ikidai kuwa vilikuwa ni vituo vya kuhamasisha ushoga.

Serikali Dar es Salaam iliahidi kuwaondoa nchini raia wa kigeni wote wanaofanya kampeni kutaka mashoga wapewe haki zao.

Ushoga kwa kukutana kimwili wanaume unaadhibiwa kwa kifungo kati ya miaka 30 hadi maisha katika Sheria za Tanzania. Hakuna katazo kama hilo kwa kosa la mapenzi baina ya wanawake.

Kwa mujibu wa Shirika la Haki za Binadamu Amesty International, ushoga ni kinyume cha sheria katika nchi 38 kati ya nchi za Kiafrika 54 na adhabu yake ni kifo huko Mauritania, Somalia na Sudan.
Uganda in 2014 tried to impose the death penalty on those found guilty of being homosexual, however the controversial law was later repealed.

Uganda mwaka 2014 ilijaribu kuweka adhabu ya kifo kwa wale watakao kutinakana na kosa la kujihusisha na ushoga , lakini sheria hiyo tata iliondolewa kabisa siku za usoni.

XS
SM
MD
LG