Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Januari 22, 2025 Local time: 00:04

Lebanon: Afisa mstaafu avamia benki akiomba kupewa pesa zake dola 24,000


Mteja wa benki akiwarushia mayayi walinzi wa benki, wakati wa maandamano mjini Beirut, Oktoba 6, 2021. Picha ya AP
Mteja wa benki akiwarushia mayayi walinzi wa benki, wakati wa maandamano mjini Beirut, Oktoba 6, 2021. Picha ya AP

Afisa mstaafu wa Lebanon Jumanne ameivamia benki moja akiomba kutuma pesa kwa mtoto wake anayesoma nchini Ukraine, shirika la kutetea wateja limesema, ikiwa mojawapo ya benki tatu zilizovamiwa na wateja nchini Lebanon.

Benki nchini humo, zinazokumbwa na mzozo wa kiuchumi kwa zaidi ya miaka miwili, zilifunguliwa kwa muda wiki iliyopita chini ya ulinzi mkali baada ya kufungwa kwa wiki nzima kufuatia uporaji mwingi wa wateja waliokata tamaa ya kupata pesa zao.

Ali Deeb al Sahili alilishikilia mateka tawi la benki moja katika mji wa Chatura ulio umbali wa kilomita 45 mashariki mwa mji mkuu Beirut, kulingana na shirika linalotetea wateja wa benki, akitaka kutuma pesa kwa mwanawe nchini Ukraine.

Mwanajeshi huyo aliyestaafu ambaye alikuwa na silaha, mwenye umri wa miaka 50, aliomba kupewa dola 24,000 zinazohifadhiwa kwenye akaunti yake.

Kaka yake amesema aliwekwa kizuizini, na haikufamika wazi ikiwa alifanikiwa kupata pesa yoyote ya akiba yake.

XS
SM
MD
LG