Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 12:53

Korea Kaskazini yarusha tena makombora


North Korean leader Kim Jong Un salutes as he arrives to inspect a military drill at an unknown location.
North Korean leader Kim Jong Un salutes as he arrives to inspect a military drill at an unknown location.

Korea Kusini imesema kuwa Korea Kaskazini imerusha makombora ya masafa mafupi kwenye bahari karibu na ufukwe wake licha ya taifa hilo lililotengwa kuwekewa vikwazo vya kimataifa pamoja na zoezi la kijeshi linaloendelea kwa ushirikiano wa Marekani na Korea Kusini.

Wakuu wa kijeshi wa Korea Kusini wamesema kombora lilirushwa leo karibu na mji wa bandari wa Korea Kaskazini wa Wonan huku ikienda umbali wa kilomita 200 kabla ya kuanguka ardhini.

Pyongyang ilirusha makombora matano ya masafa mafupi jumatatu ya tarehe 21 Machi kwenye bahari ya mashariki kutoka kwenye mji wa Hamhung. Korea Kusini imekuwa ikitishia kurusha makombora ya nyuklia dhidi ya Washington na Seoul kama hatua ya kulalamikia zoezi la pamoja la kijeshi kati ya Marekani na Korea Kusini.

XS
SM
MD
LG