Wanadiplomasia mjini Brussels wanasema hakuna muafaka wa nani atachukua nafasi ya waziri mkuu nafasi wa zamani wa Norway, Jens Stoltenberg, ya kuwa kiongozi wa juu wa kiraia wa umoja huo wa m ushirika wa magharibi.
Baadhi ya washirika walikuwa wanafikiria kupanga kuongeza kipindi chake ambapo tayari ameshahudumu kwa miaka tisa kusimamia NATO inavyo itikia mgogoro ambao umeanzisha vita vya Russia dhidi ya Ukraine.
Lakini Jumapili, muda mfupi baada Stoltenberg kurejea toka katika mikutano ya ngazi ya juu jijini Washington, msemaji wake amethibitisha kwamba ataondoka katika wadhifa huo baadaye mwaka huu.
Facebook Forum