Moore anayeongoza idara hiyo maarufu kama SIS au M16, amesema kwamba anaamini kufufuliwa kwa mkataba wa 2015 maarufu kama JCPOA, ndiyo njia bora zaidi ya kudhibiti program ya nyuklia ya Iran. Chini ya mkataba huo, Iran ilikuwa imekubali kupunguza uzalishaji wake wa nyuklia ili kuondolewa baadhi ya vikwazo vya kiuchumi na mataifa hayo.
Tangu rais wa Marekani aliyeondoka madarakani Donald Trump kuiondoa Marekani kwenye mkataba huo 2018, Iran imekiuka masharti mengi yaliyowekwa, wakati ikiendelea kusindika uranium yenye viwango vya kutengeneza silaha. Mataifa ya magharibi yameonya kwamba Iran inakaribia kutengeneza bomu la nyuklia , suala ambalo imekanusha vikali.
Facebook Forum