“Hii ni kuwatangazia rasmi raia wenzangu wa Zimbabwe na dunia nzima, kwamba kuanzia sasa, sina uhusiano wowote tena na chama cha CCC,” Chamisa amesema katika taarifa.
Amekishtumu chama tawala cha ZANU PF cha Rais Emmerson Mnangagwa kutumia vyombo vya dola kukidhoofisha chama cha CCC.
Uamuzi huo wa kushangaza unajiri baada ya Mnangangwa, mwenye umri wa miaka 81 kushinda muhula wa pili, kwa kumshinda kiongozi huyo wa chama cha the Citizens Coalition for Change(CCC), katika uchaguzi ambao ulikipa chama tawala cha ZANU-PF wingi wa viti katika bunge.
Waangalizi wa kimataifa wamesema uchaguzi haukukidhi vigezo vya demokrasia na mvutano wa kisiasa uliongezeka tangu wakati huo.
Forum