Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 25, 2026 Local time: 18:17

Kimbunga kimesababisha vifo na uharibifu New Zealand

Mafuriko makubwa New Zealand
Mafuriko makubwa New Zealand

Waziri mkuu wa New Zealand Chris Hipkins amewaonya raia wa nchi hiyo kujitayarisha kwa uwezekano wa kuwepo vifo zaidi kutokana na kimbunga Gabrielle.

Polisi wamesema kwamba watu watano wamefariki kutokana na kimbunga hicho na kwamba huenda idadi ikaongezeka.

Onyo hilo limetokea huku shughuli za uokoaji zikiendelea, huku baadhi ya watu wakiwa hawajulikani walipo baada ya kimbunga kutokea siku tatu zilizopita.

Shughuli za uokoaji zinaendelea.

Kimbunga Gabrielle kimesababisha uharibifu mkubwa ambao haujawahi kuonekana nchini New Zealand kwa miongo kadhaa.

Hali ya dharura ilitangazwa Jumanne, na kuruhusu serikali kutoa msaada zaidi kwa watu katika sehemu zilizoathirika.

This item is part of
XS
SM
MD
LG