Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 04:29

Kiir asema kuna tishio jipya kwa umoja wa Sudan Kusini


Rais wa Sudan Salva Kiir.
Rais wa Sudan Salva Kiir.

Wakati wa maadhimisho ya miaka tisa ya uhuru wa Sudan Kusini, rais wa nchi hiyo Salva Kiir, Alhamisi alikiri kwamba miezi kadhaa ya mapigano ya ndani kwa ndani inatishia kuligawanya taifa hilo.

Katika hotuba yake ya taifa kwa njia ya televisheni, Rais Kiir alitoa wito kwa Wasudan kusini wote kufanya juhudi za kiuleta amani na maridhiano ya kijamii, akisema kuwa jamii nyingi zimegawanyika kutokana na vita.

"Ghasia za kisiasa hivi sasa hazipo. Kwa bahati mbaya, mafanikio yetu katika kumaliza ghasia za kisiasa hivi sasa yanatishiwa na aina tofauti ya ghasia," alisema Kiir.

"Mzozo wa ndani kwa ndani unaendelea katika maeneo tofauti ya nchi yetu. Kama serikali hatutaruhusu jambo kama hili kujirudia," aliongeza.

Mkuu wa ofisi za Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini, David Shearer aliiambia VOA kwamba watu wapatao mia moja walikufa mwezi uliopita katika wimbi la mashambulizi na mashambulizi ya kujibizana katika jimbo la Jonglei.

-Imetayarishwa na Mkamiti Kibayasi, VOA, Washington DC

XS
SM
MD
LG