Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 03:38

Kenyatta amewafutia adhabu ya kifo wafungwa kadhaa wa Kenya


Kenya President Uhuru Kenyatta watches 105 tons of elephant ivory and more than 1 ton of rhino horn being destroyed in a bid to stamp out the illegal ivory trade, Nairobi National Park, Kenya, April 30, 2016.
Kenya President Uhuru Kenyatta watches 105 tons of elephant ivory and more than 1 ton of rhino horn being destroyed in a bid to stamp out the illegal ivory trade, Nairobi National Park, Kenya, April 30, 2016.

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya, Jumatatu amewafutia adhabu ya kifo takriban wafungwa 2,747 ambao walikuwa wanasubiri kunyongwa na hivyo hivi sasa watatumikia kifungo cha maisha jela.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Ufaransa, Kenyatta alitia saini waraka wa kuwafutia adhabu hiyo wakati wa sherehe ambazo zilifanyika kwenye makazi yake rasmi na pia kuwasamehe wafungwa 102 ambao wamekuwa wakitumikia vifungo kwa muda mrefu.

Amnesty International imefurahishwa na hatua hiyo na kuisihi kenya kufuta rasmi adhabu ya kifo. Kenya haijawahi kunyonga mtu yoyote tangu mwaka 1987. Uamuzi wa kuwafutia adhabu ya kifo unaifanya kenya ikaribie kuifikia jumuiya ya mataifa ambayo imefuta adhabu ya kifo kwa vile ni ya kinyama na si kitendo cha kibinadamu, alisea Muthoni Wanyeki mkurugenzi wa haki za binadamu katika taasisi hiyo.

XS
SM
MD
LG