Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Mei 06, 2024 Local time: 00:13

Kenya yatoa tahadhari ya mafuriko zaidi wakati mvua zikiendelea


Watu wakiwa wamebeba mizigo yao wakivuka barakara iliyoporomoka karibu na eneo la Garissa Novemba 22, 2023. Picha na LUIS TATO / AFP.
Watu wakiwa wamebeba mizigo yao wakivuka barakara iliyoporomoka karibu na eneo la Garissa Novemba 22, 2023. Picha na LUIS TATO / AFP.

Kenya imetoa tahadhari ya mafuriko wakati mvua kubwa zikinyesha katika eneo hilo. Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya limesema mafuriko katika taifa hilo la Afrika Mashariki yameua watu 38 na zaidi ya 11,000 wamekoseshwa makazi.

Shirika hilo limesema limewaokoa watu 180 kutoka kwenye maji katika maeneo mbalimbali nchini.

Venant Ndigila, mkuu wa mipango katika shirika la kibinadamu huko Kenya, amesema mvua zimesabaisha majanga kwa Wakenya.

Misaada ya kibinadamu imejitokeza sana katika eneo hili. Na hili ni muhimu sana kuhusiana na malazi, ambapo familia hizo 11,275 …haziwezi kuzitumia nyumba zao, au zimepoteza nyumba zao” amesema Ndigila.

Kenya imeanza kupata mvua katikati ya mwezi Machi, lakini katika miezi michache iliyopita, mvua zimekuwa zikiongezeka kwa kiwango kikubwa.

Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya limesema zaidi ya milimita 100 za mvua zimerekodwa katika maeneo mengi nchini humo katika kipindi cha wiki iliyopita, na kusababisha vifo vya watu sita.

Forum

XS
SM
MD
LG