Swala la ziara za kiserikali za Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta zimezua majadala mkali miongoni mwa wakenya katika siku za hivi karibuni.
Baadhi ya wakenya wanaunga mkono ziara hizo wakidai kuwa zinaleta manufaa kwa taifa huku wengine wakidai ni matumizi mabaya ya fedha za umma kwa nchi hiyo ambayo bado inachipukia kiuchumi.
Navyo vyama vya upinzani pamoja na baadhi ya mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali yalidai kuwa zaidi ya shilingi bilioni 2.1 tayari zimetumika katika ziara hizi za Rais pamoja na Makamu Rais, William Ruto.