Kenya imeandaa kongamano ligine la kujadili tendo la ugaidi kwa kuchunguza kiini cha uovu huo na athari zake, yakiwepo mazungumzo yaliyoshirikisha viongozi mbali-mbali, taasisi pamoja na wasomi.
Kongamano hilo katika mji mkuu wa Nairobi limeandaliwa wakati Kenya ikiomboleza wanajeshi wake waliouawa wiki mbili zilizopita na magaidi wa Al Shabaab,walipokuwa wakilinda amani nchini Somalia.
Kongamano hilo linakuja muda mfupi baada ya Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari na mwenzake wa Somalia Hussein Sheikh kuzulu Kenya na kuahidi kushirikiana na Kenya kwenye vita dhidi ya Ugaidi.