Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 21, 2025 Local time: 02:43

Katibu mkuu wa NATO: Kuna ishara kuwa China inapanga kuiunga mkono Russia katika vita vya Ukraine


Katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg
Katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg

Mkuu wa NATO Jumatano amesema muungano huo wa kijeshi umeona baadhi ya ishara kwamba China inaweza kuwa inapanga kuiunga mkono Russia katika vita vyake dhidi ya Ukraine, na kuitaka Beijing kuachana na kile ambacho amesema, kitakuwa ukiukaji wa sheria za kimataifa.

Katibu mkuu wa NATO Jens Stoltenberg ameiambia pia AP katika mahojiano kwamba muungano huo, ingawa haushiriki katika vita, utaiunga mkono Ukraine“kwa muda mrefu utakaohitajika.”

Akiulizwa iwapo NATO ina dalili zozote kwamba China inaweza kuwa tayari kutoa silaha au msaada mwengine kwa vita vya Russia, Stoltenberg amesema “ Tumeona baadhi ya ishara kwamba wanaweza kupanga hilo na bila shaka washirika wa NATO, Marekani, wamekuwa wakionya dhidi ya hilo kwa sababu ni jambo ambalo halipaswi kutokea. China haipaswi kuunga mkono vita haramu vya Russia.”

XS
SM
MD
LG