Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Juni 22, 2025 Local time: 04:26

Kamanda wa Hezbollah auwawa kwenye shambulizi la Israel kusini mwa Lebanon


Moshi kutokana na mashambulizi ya Israel dhidi ya kijiji kimoja kusini mwa Lebanon. Picha ya mkataba.
Moshi kutokana na mashambulizi ya Israel dhidi ya kijiji kimoja kusini mwa Lebanon. Picha ya mkataba.

Jeshi la Israel limesema Jumatatu kwamba limefanya shambulizi la anga kusini mwa Lebanon, ambalo limeua kamanda mmoja wa kundi la Hezbollah aliyeongoza mashambulizi kadhaa yakilenga kaskazini mwa Israel.

Taarifa kutoka jeshi hilo imemtambulisha kamanda huyo kama Ali Ahmad Hassin, kutoka kikosi cha Hezbollah cha Radwan. Kundi hilo la wapiganaji pia limetangaza kifo cha mpiganaji wake kwa jina hilo hilo, bila kutoa maelezo zaidi. Taarifa kutoka kwa jeshi la Israel zimeongeza kuwa shambulizi hilo pia limeua watu wengine wawili.

Mashambulizi ya mpakani kati ya vikosi vya Israel na wapiganaji wa Hezbollah yamekuwa jambo la kawaida kwa miezi 6 sasa, tangu kuzuka kwa vita kati ya Israel na kundi la Hamas linaloungwa mkono na Hezbollah, huko Ukanda wa Gaza. Kwenye taarifa tofauti, jeshi la Isreal limesema kwamba limefanya mashambulizi ya anga huko Khan Younis kusini mwa Gaza, yakiwa majibu kutokana na mashambulizi kadhaa ya roketi kutoka Hamas.

Maafisa wa Israel Jumapili walitangaza kuondolea vikosi vyake kutoka Khan Younis. Waziri wa Ulinzi wa Israel Yoav Gallant amesema kuwa vikosi hivyo vimeondolewa wakati vikijitayarisha kuanza operesheni nyingine, inayojumuisha kuingia mji wa Rafah.

Forum

XS
SM
MD
LG