Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 19:10

Zitto Kabwe akosoa serikali inavyo kabiliana na janga la Corona


Zitto Kabwe, Mbunge wa ACT- Wazalendo akitoa hoja bungeni.
Zitto Kabwe, Mbunge wa ACT- Wazalendo akitoa hoja bungeni.

Kiongozi wa chama cha upinzani - ACT Wazalendo, Zitto Kabwe anasema ikiwa watu hawatafuata miongozo inayotolewa na Shirika la Afya Duniani kuna hatari ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosababishwa na virus vya corona kusambaa kwa haraka kote nchini.

Katika mahojiano siku ya Alhamisi Kabwe alikosoa msimamo wa Rais Magufuli wa kukataa kufunga shughuli zote za biashara na utawala katika miji ambayo kuna uambukizaji mkubwa zaidi kama vile Dar es Salaam, kama wanavyofanya nchi nyingine duniani.

Akiwahutubia viongozi wa usalama nchini siku ya Juamtano Rais Magufuli alisema," wapo wengine wanatoa mawazo ya kuifunga Dar es Salaam, hili haliwezekani. Dar es salam ndio centre pekee ambapo collection ya revenue inapatikana kwa nchi yetu"

COVID-19 : ACT yaishauri serikali ya Tanzania ifuate muongozo wa WHO
please wait

No media source currently available

0:00 0:07:36 0:00

Kiongozi wa ACT Mzalendo anasema kwamba ni kweli kuna baadhi ya nchi ambazo haziwezi kusitisha shughuli zote za kiuchumi, lakini kulingana na Benki Kuu ya Dunia, "Tanzania inauwezo wa kufunga shughuli kwa kiwango fulani na serikali ikawafidia wananchi na kuwalipa."

Anasema akiba ya fed za kigeni ya Tanzania inaweza kutosha kuendesha nchi kwa zaidi ya miezi sita bila ya shughuli zozote kufanyika.

Imetayarishwa na Mwandishi wetu, Abdushakur Aboud, Washington, DC

XS
SM
MD
LG