Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Januari 16, 2025 Local time: 07:27

Juhudi za kumkamata Rais wa Korea Kusini zakwama


Wachunguzi wa kupambana na ufisadi wakiondoka kwenye makazi ya Rais wa Korea Kusini aliyeondolewa na bunge Yoon Suk Yeol, Januari 3, 2025. Picha ya AFP
Wachunguzi wa kupambana na ufisadi wakiondoka kwenye makazi ya Rais wa Korea Kusini aliyeondolewa na bunge Yoon Suk Yeol, Januari 3, 2025. Picha ya AFP

Mamlaka za Korea Kusini Ijumaa zimesimamisha jaribio la kumkamata Rais aliyeondolewa baada ya kushtakiwa na bunge Yoon Suk Yeol kufuatia hali ya mvutano mkali wa saa sita kati ya wachunguzi na maafisa wa usalama watiifu kwa rais huyo.

Katika taarifa, timu ya pamoja ya uchunguzi iliyojaribu kumkamata Yoon ilisema “ilikuwa haiwezekani kabisa” kuendelea na utekelezaji wa hati ya kumkamata iliyoidhinishwa na mahakama kwa kuzingatia upinzani na usalama wa wafanyakazi kwenye eneo la tukio.

Katika operesheni ya mapema asubuhi, timu ya wachunguzi na maafisa wa upelelezi, wakiungwa mkono na polisi wa kutuliza ghasia wapatao 3,000, walifika kwenye makazi ya Yoon katikati mwa Seoul, kama sehemu ya uchunguzi kuhusu uasi na matumizi mabaya ya madaraka.

Forum

XS
SM
MD
LG