Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 09:13

Japan imeonya China kutokana na uchokozi katika mipaka yake


Waziri mkuu wa Japan Fumio Kishida akifuatilia mazungumzo katika kongamano la 25 la nchi za ASEAN, mjini Phnom, Cambodia. Nov 12, 2022
Waziri mkuu wa Japan Fumio Kishida akifuatilia mazungumzo katika kongamano la 25 la nchi za ASEAN, mjini Phnom, Cambodia. Nov 12, 2022

Waziri mkuu wa Japan Fumio Kishida, amewaambia viongozi wa mataifa ya Asia kwamba China inaendela kuchukua hatua ambazo zinaingilia uhuru na mipaka ya Japan, na huenda hatua hizo zikasababisha mivutano katika eneo hilo.

Katika hotuba yake kwa viongozi wanaohudhuria kongamano la ASEAN nchini Cambodia, Kishida amesema kwamba ni muhimu kuhakikisha kwamba kisiwa cha Taiwan kina amani na utulivu, kwa maslahi ya usalama wa eneo hilo.

Ameendelea kusema kwamba kuna wasiwasi mkubwa kuhusiana na ukandamizaji wa haki za kibinadamu dhidi ya watu wa Uyghur.

Taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya Japan imesema kwamba China imekuwa ikichukua hatua za kichokozi katika bahari ya East China, na zinazoingilia uhuru wa Japan, na kuendelea kuongeza mivutano katika eneo hilo.

Matamshi ya Kishida yanafuatia msimamo wa rais wa Marekani Joe Biden aliyesisitiza kwamba viongozi wa Asia wanastahili kuhakikisha kwamba kuna amani katika kisiwa cha Taiwani na kuhakikisha kwamba kuna uhuru wa usafiri katika bahari ya South China.

Kishida pia amesema kwamba hatua ya Korea Kaskazini kuendelea kufanya majaribio ya makombora ya masafa marefu, ikiwemo kombora lililopaa juu ya Japan, hayakubaliki.

XS
SM
MD
LG