Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 20, 2025 Local time: 10:10

Jamuhuri ya Czech kufungua kituo Taiwan


Jamhuri ya Czech, Jumatatu imesema itafungua kituo kipya cha kuimarisha uhusiano wa kitamaduni na kidiplomasia katika mji mkuu wa Taiwan, Taipei, wiki hii, hatua ambayo huenda ikaikasirisha China.

China inatambua Taiwan kuwa ni sehemu yake chini ya sera ya China moja, na mwezi uliopita ilizindua mazoezi ya kijeshi kuzunguka kisiwa hicho kinachojitawala.

Jamhuri ya Czech, Umoja wa Ulaya na mwanachama wa NATO, inaafiki sera ya China moja, kama EU, lakini maafisa wake wanaendeleza uhusiano wa karibu na Taiwan.

“Kituo cha Czech, nchini Taiwan kitazindua shughuli zake Ijumaa, Juni 14, kwa maonyesho ya picha za Kczech, wizara ya mambo ya nje imeeleza.

Shirika la habari la CTK limemnukuu mkuu wa kituo cha Czech, Jitka Panek Jurkova, akisema raia wa Czech, wanataka kuonekana na kusikilizwa Taipei.”

Wizara ya mambo ya nje ya Czech, ina vituo 28 vinavyotangaza taifa hilo katika nchi 25 ulimwenguni isipokuwa China.

Forum

XS
SM
MD
LG