Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 18, 2024 Local time: 08:41

Italy imewapokea wahamiaji baada ya kuwaacha katika bahari iliyochafuka kwa siku kadhaa


Meli ya uokoaji ya Geo Barents ikiwa na wahamiaji baada ya kutia nanga katika bandari ya Salerno, Italy, Dec 11, 2022
Meli ya uokoaji ya Geo Barents ikiwa na wahamiaji baada ya kutia nanga katika bandari ya Salerno, Italy, Dec 11, 2022

Serikali ya Italy, ambayo imetangaza msimamo mkali dhidi ya wahamiaji, imekubali kuwapokea wahamiaji 500, baada ya meli mbili za hisani za uokoaji kuruhusiwa kutia nanga katika bandari zake kusini mwa nchi, baada ya kuzuiliwa kwa siku kadhaa baharini licha ya hali mbaya ya hewa.

Meli ya uokoaji ya Geo Barents, inayoendeshwa na shirika la madaktari wasiokuwa na mpaka MSF, ikiwa na wahamiaji 248, iliwasili Salerno, kusini magharibu mwa Campania.

Meli nyingine ya uokoaji kwa jina Humanity 1, inayoendeshwa na shirika la msaada la SOS, imeruhusiwa na maafisa wa Italy, kuingia katika bandari ya Bari ikiwa na wahamiaji 261.

Meli hizo zilikuwa zinakabiliwa na hali mbaya ya hewa, zikipigwa na mawimbi ya bahari yenye urefu wa mita 3 na upepo mkali.

Hali ya majibizano iliongezeka kati ya Italy na Jirani yake - Ufaransa, mwezi uliopita, baada ya Ufaransa kuruhusu boti yenye wahamiaji ambayo ilikataliwa na Italy.

Maafisa wa Italy wamesema kwamba wameruhusu meli hizo kuingia katika bandari zake kutokana na hali mbaya ya hewa wala sio kwamba imebadilisha sera yake kuhusu wahamiaji.

XS
SM
MD
LG