Jeshi la Israel, idara yake ya upelelezi na kitengo maalum cha polisi walisema waliokoa watu wawili, Fernando Simon Marman mwenye umri wa miaka 60, na Louis Har mwenye umri wa miaka 70, ambao wana uraia pacha wa Israel na Argentina.
Wawili hao walikuwa miongoni mwa mateka 240 walioshikiliwa na Hamas katika shambulio la Oktoba 7 ndani ya Israel ambalo lililua watu 1,200 na kupelelea Israel kufanya mashambulizi ya kulipiza kisasi.
Miezi minne tangu vita kuzuka, maafisa wa afya huko Gaza wanasema zaidi ya Wapalestina 28,000 waliuawa na wengine 68,000 kujeruhiwa.
Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alipongeza kuokolewa kwa mateka hao na kutupilia mbali tuhuma za Jumuia ya kimataifa kuhusu mipango yake ya kufanya mashambulizi ya ardhini ili kutokomeza vikosi vine vya Hamas huko Rafah.
Forum