Israel, Jumatatu imethibitisha hatua hiyo, na kuushutumu uchunguzi huo kwa kusema itakuwa ni kosa kubwa na kuapa kutotoa ushirikiano.
Waziri wa ulinzi wa Israel Benny Gantz, alitoa taarifa hiyo kupitia mtandao wa Twitter, akisema Israel imeweka wazi kwa Marekani kwamba haitotoa ushirikiano wa uchunguzi wowote wa nje.
Amesema hawata ruhusu kuingiliwa katika masuala ya ndani ya Israel.
Mwanahabari wa Kipalestina ambaye alikuwa ana andika habari za oparesheni za Israel ndani ya Palestina, Abu Akleh, alikuwa pia raia wa Marekani.
Msemaji wa wizara ya sheria ya Marekani hakujibu lolote baada ya kuombwa kujibu taarifa ya waziri wa Israel, Gantz.
Haikuwa wazi kuhusu lini hasa uchunguzi huo unaweza kuanza, na kile kitakacho chunguzwa.
Lakini uchunguzi wa Marekani ndani ya Israel imekuwa ni jambo la nadra na linaweza kutikisa uhusiano wa mataifa hayo mawili.