Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 16, 2025 Local time: 11:49

Israel yaongeza mashambulizi yake katika Ukanda wa Gaza


Moshi unaoneakana kufuatia shambulio la Israel katika Ukanda wa Gaza, kama inavyoonekana kutoka kusini mwa Israel, Jumamosi, Desemba 2, 2023. (Picha ya AP/Leo Correa)
Moshi unaoneakana kufuatia shambulio la Israel katika Ukanda wa Gaza, kama inavyoonekana kutoka kusini mwa Israel, Jumamosi, Desemba 2, 2023. (Picha ya AP/Leo Correa)

Israel ilizidisha mashambulizi yake makubwa  ya mabomu katika Ukanda wa Gaza siku ya Jumamosi huku mapigano mapya na Hamas yakiingia siku ya pili kufuatia kuvunjika  kwa sitisho la mapigano la wiki nzima.

Maafisa wa jeshi la Israel walisema Jumamosi zaidi ya malengo 50 ya Hamas katika eneo la Khan Yunis kusini mwa Gaza yalipigwa na vikosi vya anga, majini na ardhini. Jeshi lilisema lilifanya mashambulizi kaskazini na kwamba zaidi ya malengo 400 huko Gaza yamepigwa tangu mapigano kuanza tena siku mbili zilizopita.

Ghasia za Jumamosi zilikuja siku moja baada ya mashambulizi ya anga ya Israel kwenye eneo la Palestina kuwaua watu 184, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Gaza.

Nchini Syria, Wizara ya Ulinzi ilisema Israel ilifanya mashambulizi ya anga karibu na Damascus mapema Jumamosi. Vyombo vya habari vya serikali ya Syria viliripoti kwamba vyombo vya ulinzi wa kijeshi viliangusha makombora mengi ya Israeli. Ilisema hakuna ripoti za majeruhi.

Forum

XS
SM
MD
LG