Sheria za Israel haziharamishi bendera za Palestina lakini polisi wana haki ya kuziondoa katika matukio ambapo wanaona kuna tishio kwa usalama wa umma.
Maagizo kutoka kwa Ben-Gvir, ambaye anaongoza chama chenye msimamo mkali katika serikali mpya ya Benjamin Netanyahu na kama waziri anayesimamia polisi, yanaonekana kuchukua msimamo mkali kutaka bendera hizo ziondolewe.
Agizo hilo linafuatia kuachiliwa wiki iliyopita kwa mfungwa wa Kipalestina wa muda mrefu, aliyepatikana na hatia ya kumteka nyara na kumuua mwanajeshi wa Israel mwaka 1983, ambaye alipeperusha bendera ya Palestina akipokelewa kama shujaa katika kijiji chake kaskazini mwa Israel.
Katika taarifa, Ben-Gvir alisema kupeperusha bendera ya Palestina ni kitendo cha kuunga mkono ugaidi.
Facebook Forum