Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Januari 18, 2025 Local time: 17:44

Israel imetoa amri kwa Wapalestina kuondoka kwenye maeneo ili kufanya mashambulizi


Israel imetoa amri mpya kwa Wapalestina wasiokuwa na  makazi kusini mwa Gaza, Jumapili wakati mapigano yakipamba moto baada ya kuvunjika kwa makubaliano ya kusimamisha mapigano na wanamgambo wa Hamas, Ijumaa.

Kwa kutumia lugha ya kiarabu katika kurasa za mitandao ya Facebook na X, Israel imewaambia Wapalestina kwamba kuheshimu amri hiyo ni jambo la usalama kwa maisha yao na familia zao.

Wengi wa Wapalestina wametakiwa kuondoka kaskazini mwa Gaza, mapema katika vita vya miezi miwili na Hamas.

Kutokana na uwezekano wa mashambulizi zaidi katika eneo hilo Israel imewaeleza Wapalestina kuondoka katika maeneo 34 ambayo yote yanapatikana kusini mwa mji wa Khan Younis, na kuelekea katika eneo ambalo limeshajaa kuhifadhi watu ama kile kinachoitwa ukanda wa kibinadamu uliopo Al Mawasi, eneo la kilimo ambalo lipo karibu na bahari ya Mediterranean.

Forum

XS
SM
MD
LG