Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 08:30

ISIS yathibitisha kifo cha kiongozi wake


Bendera ya ISIS, picha ya Reuters.
Bendera ya ISIS, picha ya Reuters.

Kundi la Islamic State Alhamisi limethibitisha kifo cha kiongozi wake Abu Hussein al-Hussein al-Quraishi na limemteua Abu Hafs al-Hashimi al-Quraishi kama kiongozi wake mpya, msemaji wa kundi hilo alisema katika sauti kwenye mtandao wa Telegram wa kundi hilo.

Limeonekana kuwa tangazo la kwanza rasmi la kundi hilo kuhusu hatma ya kiongozi wake tangu Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki aliposema mwezi Aprili kwamba maafisa wa ujasusi wa Uturuki walimuua kiongozi huyo wa ISIS nchini Syria.

Kundi hilo lilipata nguvu mwaka 2014 wakati kiongozi wake wa wakati huo, Abu Bakr al-Baghdadi, alipotangaza eneo linalodhibitiwa na kundi hilo kuwa chini ya sheria kali za kiislamu.

Abu Hussein al-Hussein al-Quraishi alichukua uongozi wa ISIS mwezi Novemba mwaka 2022, baada ya mtangulizi wake kuuawa pia nchini Syria.

Forum

XS
SM
MD
LG