Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 23, 2025 Local time: 11:52

Ireland, Spain na Norway kutambua Palestina kama taifa kamili


Waziri mkuu wa Norway Jonas Gahr Store akihutubia waandishi wa habari mjini Oslo
Waziri mkuu wa Norway Jonas Gahr Store akihutubia waandishi wa habari mjini Oslo

Ireland, Spain na Norway zimetangaza kwamba zitaanza kuitambua Palestina kuwa nchi kamili kuanzia Mei 28 na kuongezea kwamba zinatarajia kwamba nchi nyingine za Magharibi zitafuata mkondo huo.

Israel imekasirishwa na hatua hiyo na kuwaita mabalozi wake katika nchi hizo kurudi Israel.

Waziri mkuu wa Spain Pedro Sanchez ameitaja hatua hiyo kuwa yenye lengo la kushinkiza kusitishwa vita kati ya Israel na wanamgambo wa Hamas huko Gaza.

Israel ilianzisha operesheni ya kijeshi huko Gaza kujibu mashambulizi ya Hamas yaOktoba 7 yaliyoua watu 1200 na kutekwa nyara watu 250.

Kulingana na wizara ya afya ya Gaza, mashambulizi ya Israel katika eneo hilo yameua watu zaidi ya 35,000.

Spain imekuwa ikishawishi mataifa ya Ulaya yakiwemo Ufaransa, Ureno, Ubelgiji na Slovenia kuunga mkono juhudi za kuitambua Palestina kama taifa kamili.

Forum

XS
SM
MD
LG