Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Januari 18, 2025 Local time: 17:58

Iraq : Vikosi vya usalama vyawatawanya waandamanaji kwa risasi na mabomu ya machozi


Waandamanaji wakitawanyika wakati vikosi vya usalama nchini Iraqi walipotupa mabomu ya machozi katika maandamano yanayo kosoa serikali kutokana na kukosekana ajira, rushwa na huduma mbaya za umma, Baghdad, Iraq Octoba 2, 2019. REUTERS/Khalid al-Mousily -
Waandamanaji wakitawanyika wakati vikosi vya usalama nchini Iraqi walipotupa mabomu ya machozi katika maandamano yanayo kosoa serikali kutokana na kukosekana ajira, rushwa na huduma mbaya za umma, Baghdad, Iraq Octoba 2, 2019. REUTERS/Khalid al-Mousily -

Vikosi vya usalama Iraq vilitumia mabomu ya machozi na risasi za moto kutawanya waandamanaji katika mji mkuu wa Baghdad. 

Waziri mkuu Adel Abdul-Mahdi alitangaza marufuku ya kutembea nje kama namna ya kudhibiti maandamano hayo katika mji mkuu na maeneo mengine ya nchi.

Tangu maandamano hayo yaanze watu 18 wamepoteza maisha ikiwa ni pamoja na polisi mmoja na mamia kujeruhiwa.

Pamoja na risasi za moto na mabomu ya machozi polisi hao wameweka mapipa ya maji na risasi za bandia ili kujaribu kuvunja maandamano hayo.

Waandamanaji wamechukizwa na huduma hafifu za serikali na rushwa.

Imetayarishwa na mwandishi wetu, Washington, DC.

XS
SM
MD
LG