Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 16, 2025 Local time: 22:02

Iran yathibitisha imewahamisha wafungwa wanne wa Marekani kwenye kifungo cha nyumbani


Mwanamke mmoja akiingia kwenye mlango ambao umefunikwa na picha inayoonyesha mateka wa Marekani na wafungwa ambao wanazuiliwa nje ya nchi, Jumatano, Julai 20, 2022, katika kitongoji cha Georgetown, Washington.
Mwanamke mmoja akiingia kwenye mlango ambao umefunikwa na picha inayoonyesha mateka wa Marekani na wafungwa ambao wanazuiliwa nje ya nchi, Jumatano, Julai 20, 2022, katika kitongoji cha Georgetown, Washington.

Iran imesema  makubaliano hayo na Marekani yalihusisha kati ya dola bilioni 6 na bilioni 7 ambazo zimesitishwa kutokana na vikwazo.

Iran ilithibitisha siku ya Alhamisi kwamba imewahamisha wafungwa wanne wa Kimarekani kwenye kifungo cha nyumbani baada ya mabadilishano ya mabilioni ya dola zilizozuiliwa Korea Kusini jambo ambalo linakuja wakati Tehran kwa miezi kadhaa ikionyesha kuwa iko tayari kubadilishana wafungwa na Washington.

Chini ya makubaliano hayo yaliyosimamiwa na nchi ya tatu raia wa Irani watano waliofungwa nchini Marekani wataachiliwa huru na fedha za Iran zilizozuiliwa nchini Korea Kusini zitatolewa na kuhamishiwa nchini Qatar, Tehran alisema kwa mujibu wa shirika la habari la serikali ya Iran -IRNA.

Iran imesema makubaliano hayo na Marekani yalihusisha kati ya dola bilioni 6 na bilioni 7 ambazo zimesitishwa kutokana na vikwazo.

Forum

XS
SM
MD
LG