Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatano, Juni 18, 2025 Local time: 14:04

Iran yatakiwa kutoa ushirikiano na shirika la nguvu za Atomik


Shirika la usimamizi wa nyuklia la Umoja wa Mataifa lenye waangalizi 35 (IAEA) lilipitisha azimio la kuitaka Iran kutoa ushirikiano wa uchunguzi wa shirika hilo.

Uchunguzi unahusu athari za uranium katika maeneo matatu ambayo hayajatangazwa, wanadiplomasia katika kura ya faragha ya Alhamisi walisema.

Azimio hilo lililoandaliwa na Marekani, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani linasema ni muhimu na haraka Iran ieleze asili ya chembechembe za uranium na kwa ujumla zaidi kuipa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki majibu yote inayohitaji.

Ingawa haikuwa azimio la kwanza ambalo bodi hiyo imepitisha dhidi ya Iran kuhusu suala hilo lingine lilipitishwa mwezi Juni maneno yake yalikuwa na nguvu zaidi na yaliashiria kuongezeka kwa kidiplomasia siku zijazo.

XS
SM
MD
LG