Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Juni 21, 2025 Local time: 17:25

Iran na Sweden  zimekubaliana kubadilishana wafungwa


Mchoro wa chumba cha mahakama uliotengenezwa Novemba 23, 2021 na Anders Humlebo ukimuonyesha afisa wa zamani wa gereza la Iran, Hamid Noury ​​(kushoto) na wakili Thomas Soderqvist wakati wa kesi ya uhalifu wa kivita dhidi ya Noury ​.
Mchoro wa chumba cha mahakama uliotengenezwa Novemba 23, 2021 na Anders Humlebo ukimuonyesha afisa wa zamani wa gereza la Iran, Hamid Noury ​​(kushoto) na wakili Thomas Soderqvist wakati wa kesi ya uhalifu wa kivita dhidi ya Noury ​.

Iran na Sweden  zimekubaliana kubadilishana wafungwa kumwachilia huru Hamid Nouri, aliyepatikana na hatia ya uhalifu wa kivita na Sweden  katika mauaji ya halaiki ya mwaka 1988 katika Jamhuri ya Kiislamu.

Kwa kubadilishana, Iran siku ya Jumamosi imemwachilia huru Johan Floderus, Msweden ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye taasisi ya kidiplomasia ya Umoja wa Ulaya, pamoja na mtu aliyetambuliwa kama Saeed Azizi na Waziri Mkuu wa Sweden Ulf Kristersson.

Maafisa wa Sweden hawakukubali mpango huo mara moja. Oman ilisimamia mabadilishano hayo, Shirika la Habari la Oman liliripoti. Televisheni ya taifa ya Iran iliripoti kuwa Nouri alikuwa tayari amekwishaachiliwa huru na anarejea Tehran. Mwaka 2022, Mahakama ya Wilaya ya Stockholm ilimhukumu Nouri kifungo cha maisha jela kwa kuhusika kwake katika mauaji hayo.

Forum

XS
SM
MD
LG