Polisi nchini Rwanda imepokea kwa mikono miwili uamuzi wa polisi ya kimataifa Interpol tawi la Madrid Uhispania wa kufuta kabisa waranti za kuwamakata maafisa wakuu 40 kwenye jeshi la Rwanda.Jaji mmoja nchini Spain alitoa waranti huo mwaka 2008 akiwashutumua mafias hao kutenda makosa ya ukiukaji wa haki za binadamu.
Uamuzi wa kufuta kibali cha kukamatwa kwa maafisa hao umekuja miezi michache baada ya mahakama kuu mjini Madrid Uhispania wa kufuta vibali hivyo kwa madai kwamba uchunguzi ulionyesha havina uhalali wa kuendelea kuwepo.
Hii ni mara ya pili zikisikika taarifa za kufutwa kwa vibali hivyo. Mara ya kwanza ilikuwa mwezi juni mwaka 2012.
Miaka mitatu baadaye lakini polisi nchini Uingereza ilimkatamata mkuu wa kitengo cha ujasusi nchini Rwanda liyekuwa amesafiri nchini humo kikazi, suala ambalo lilizusha maandamano makubwa mjini Kigali kupinga kitendo hicho cha polsii ya Uingereza.