Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 16, 2025 Local time: 02:03

India: Wakulima wanaoandamana wakata mazungumzo na serikali


Wakulima wa India wanaotaka kuandamana hadi New Delhi wapambana na polisi.
Wakulima wa India wanaotaka kuandamana hadi New Delhi wapambana na polisi.

Polisi nchini India wametumia gesi ya kutoa machozi na maji ya kuwasha kuwatawanya maelfu ya wakulima waliokuwa wanajaribu kuandamana hadi mji mkuu wa New Delhi baada ya kukataa pendekezo la serikali kuhusu bei ya mazao yao.

Maandamano hayo yamepelekea shinkizo la kufanyika mazungumzo mapya.

Wakulima hao, wengi wao kutoka jimbo la kaskazini la Punjab, wamekuwa wakitaka bei za mazao kuongezwa, sawa na kuwepo sheria inayosimamia mazao yao.

Idadi kubwa ya wapiga kura wanaomuunga mkono waziri mkuu Narendra Modi ni wakulima, na Modi anajaribu kutimiza matakwa yao kabla ya uchaguzi wa mwezi May.

Waziri wa kilimo Arjun Munda ameandika ujumbe kwenye mtandao wa X kwamba serikali iko tayari kwa mazungumzo na wakulima na kwamba amewaalika kiongozi wao kwa mazungumzo zaidi.

Forum

XS
SM
MD
LG