Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Juni 19, 2025 Local time: 14:42

Idadi ya vifo shambulizi la Somalia yaongezeka


Mlipuko wa bomu huko Somalia, Oktoba 14, 2017
Mlipuko wa bomu huko Somalia, Oktoba 14, 2017

Idadi ya vifo katika shambulizi lililosababisha vifo vingi nchini Somalia imeongezeka na kufikia 358 huku darzeni kadhaa bado wamepotea.

Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed atatangaza “hali ya kivita” dhidi ya kundi lenye msimamo mkali wa ki-Islam la al-Shabab lililodai kuhusika kufanya shambulizi hilo Waziri Mkuu wa Somalia alisema.

Marekani inatarajiwa kusaidia katika juhudi mpya za mapigano ambazo Rais wa Somalia Mohamed Abdullahi Mohamed amepanga kuzianzisha Jumamosi, ofisa mmoja wa jeshi la Somalia aliliambia shirika la habari la Associated Press-AP. Ofisa huyo alizungumza kwa sharti la kutotajwa jina kwa sababu alikuwa hajapewa mamlaka ya kuzungumza na waandishi wa habari.

Wakati huo huo msemaji wa jeshi la Somalia Kapteni Abdullahi Iman alisema mapigano yanayojumuisha maelfu ya wanajeshi yatajaribu kuwafurumusha wapiganaji wa kundi la al-Shabaab nje ya ngome zao katika maeneo ya Lower Shabelle na Middle Shabelle mahala ambako yanatokea mashambulizi mengi yanayosababisha vifo kwenye mji mkuu wa Somalia, Mogadishu na kwenye vituo vya jeshi la Somalia na Umoja wa Afrika.

XS
SM
MD
LG