Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 11:02

Gambia kumfungulia mashtaka rais wwa zamani Yahya Jammeh


Aliyekuwa rais wa Gambia Yahya Jammeh wakiwa na walinzi wake Nov 29 2016. PICHA; AFP
Aliyekuwa rais wa Gambia Yahya Jammeh wakiwa na walinzi wake Nov 29 2016. PICHA; AFP

Serikali ya Gambia imesema kwamba imekubali mapendekezo ya tume ya ukweli na maridhiano kwamba rais wa zamani wa nchi hiyo Yahya Jammeh anastahili kufunguliwa mashtaka ya mauaji na makosa mengine ya uhalifu wakati alipokuwa madarakani

Mwanasheria mkuu Dawda Jallow, amesema kwamba mwendesha mashtaka maalum atasimamia kesi za matumizi mabaya ya madaraka wakati wa utawala wa Jammeh, kati yam waka 1994 na 2017.

Kesi hiyo zimeorodheshwa katika ripoti ya tume ya ukweli na maridhiano iliyozinduliwa mwaka uliopita.

Tume hiyo huru ilisema kwamba Jammeh na watu aliokuwa nao serikalini, walihusika na makosa ya uhalifu 44, yakiwemo mauaji na unajisi, dhidi ya waandishi wa habari, wanajeshi, na wanasiasa wa upinzani.

XS
SM
MD
LG