Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 27, 2025 Local time: 12:59

Furaha na huzuni zadhihiri katika Bustani ya Mtakatifu Petro baada ya kusikia sauti ya Papa


(FILES) Papa Francis
(FILES) Papa Francis

Waumini wa kanisa katoliki wamekuwa na hisia mchanganyiko baada ya kusikia sauti ya Papa Francis leo Ijumaa, kwa mara ya kwanza tangu alipolazwa hospitali, mwezi Februari.

Waumini wakihudhuria ibada maalum kumuombea Papa Francis katika Bustani ya Mtakatifu Petro, Vatican, March 3, 2025.
Waumini wakihudhuria ibada maalum kumuombea Papa Francis katika Bustani ya Mtakatifu Petro, Vatican, March 3, 2025.

Sauti ya Francis, iliyorekodiwa jana Alhamisi, ilichezwa kwa waumini
waliokusanyika kwenye bustani ya Mtakatifu Petro, kwa maombi.
Vatican imesema Papa Francis mwenye umri wa miaka 88 amekuwa na
usiku mtulivu na amelala salama, aliamka baada ya saa mbili asubuhi
Ijumaa.

Madaktari wamesema hawatarajii kutoa ripoti ya hivi punde kuhusu afya
ya Papa, hadi kesho Jumamosi, kwa sababu hali yake ni thabithi na
kwamba hana matatizo ya kupumua au matatizo mengine kwa siku
kadhaa sasa.

Forum

XS
SM
MD
LG