Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 10:06

EU yaiwekea vikwazo zaidi Russia


Umoja wa Ulaya, (EU), Jumatatu umeiwekea Russia, vikwazo vipya kutokana na vita vyake dhidi ya Ukraine, ikilenga sekta ya almasi yenye faida kubwa, maafisa na mashirika zaidi ya 140, na kuziba mianya ambayo Moscow imeitumia kukwepa vikwazo vya awali.

Ni duru ya 12 ya vikwazo ambavyo EU imeiwekea Russia, toka rais Vladimir Putin, kuamuru wanajeshi wake kuingia Ukraine takriban miaka miwili iliyopita.

Hatua hizo zimelenga sekta ya nishati, benki, makampuni na masoko, pamoja na kuwazuia maafisa 1,000 wa Russia, kusafiri.

Makao makuu ya Umoja wa Ulaya yamesema hatua za sasa ni pigo zaidi kwa uwezo wa rais Putin, wa kuendeleza vita kwa kulenga sekta muhimu katika uchumi wa Russia, na kuifanya iwe vigumu zaidi kukwepa vikwazo vya Umoja wa Ulaya.

Uagizaji, ununuzi ama usafirishaji wa almasi asilia na vito vya almasi zisizo za viwandani utapigwa marufuku kuanzia Januari 1.

Forum

XS
SM
MD
LG