Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Aprili 23, 2024 Local time: 16:56

Dola bilioni 1 zachangishwa kwa ajili ya kuijenga tena Ukraine


Watu wakibeba vitu vyao kutoka kwa nyumba iliyoharibiwa Ukraine, kutokana na mashambulizi ya makombora ya Russia katika mji wa Vyshgorod, Ukraine, Nov. 24, 2022.
Watu wakibeba vitu vyao kutoka kwa nyumba iliyoharibiwa Ukraine, kutokana na mashambulizi ya makombora ya Russia katika mji wa Vyshgorod, Ukraine, Nov. 24, 2022.

Karibu nchi 70 na taasisi kadhaa zimeahidi msaada wa zaidi ya dola bilioni 1 kwa ajili ya Ukraine ili kusaidia katika kukarabati miundo mbinu i ambayo imeharibiwa kutokana na mashambulizi ya makombora ya Russia.

Uharibifu huo umepelekea kukatika kwa huduma ya umeme na maji kwa mamilioni ya watu wa Ukraine huku msimu wa baridi kali ukiwa umeanza.

Waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa Catherine Colonna amesema kwamba pesa hizo zimetolewa kutoka kwa wahisani wapya na kwa nia njema na waa sio mkopo.

Amesema kwamba msaada huo utaanza kutumika katika muda wa siku chache zijazo ili kuimarisha mifumo muhimu.

Karibu dola milioni 400 zitatumika kutengeneza mfumo wa nshati wa Ukraine ambao Russia imekuwa ikilenga zaidi kwa makombora.

Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy aliambia viongozi wa G7 kwamba nchi yake ilihitaji msaada wa kifedha usiopungua dola milioni 840.

XS
SM
MD
LG