Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, Compaore anatarajiwa nchini Alhamisi au Ijumaa ambapo atalakiwa na kiongozi wa taifa, chini ya mpango wa maridhiano ya kitaifa.
Mjumbe aliyetumwa na kiongozi wa kijeshi kundi linaloongoza taifa hilo Paul Henri Damiba alikutana na Compaore wiki iliyopita mjini Abidjan, wakati taarifa zikisema kwamba rais wa Ivory Coast Alassane Ouattara pia alimpokea kiongozi huyo.
Wakati akiwa Burkina Faso, Compaore atakaa kwenye nyumba ya serikali ambako rais Roch Marc Kabore alikuwa ameshikiliwa tangu kuondolewa madarakani Januari.