Serikali Jumanne imesema kwamba utaratibu wa kuingia bila visa utaanza tena kwa maeneo kama vile kisiwa cha Hainan, na pia meli zinazoingia katika jiji la bandari kuu la Shanghai, ambazo hazikuwa na mahitaji ya visa kabla ya janga hilo.
Wageni ambao walipewa visa kabla ya Machi 28, 2020, wakati Beijing ilifunga mipaka yake kwa wageni, sasa wataruhusiwa kuzitumia kuingia nchini ilimradi hazijaisha muda wake.
Kuingia bila Visa pia kutaanza tena kwa wageni kutoka Hong Kong na Macau ikiwa pamoja kuingia jimbo la kusini la Guangdong.
Beijing, Desemba ilimaliza ghafla mkakati madhubuti wa kutokomeza kabisa Covid-19, uliowekwa kwa mara ya kwanza mwanzoni mwa janga hilo.
Facebook Forum