Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 13:30

China imeanza tena safari za reli za mwendokasi


Kufunguliwa tena safari hizo kunakuja wakati ambapo kuna maambukizi makubwa yaliyojitokeza na mamlaka zinasema takriban watu 60, 000 waliokuwa na COVID- 19 wamekufa katika hospitali kufuatuilia serikali kubadilisha sera ya “ Zero- COVID” mwezi uliopita baada ya maandamano makubwa kuzuka nchini humo kuipinga.

Licha ya kuwepo na maambukizi, baadhi ya wasafiri wameeleza kufurahishwa kwao kuanza tena harakati na kufunguliwa hatua inayowawezesha kurejea katika miji yao waliokozaliwa wakati huu wa maandalizi ya sikukuu ya mwaka mpya” Lunar New Year” .

Mang Lee mwenye umri wa miaka 33 mmoja wa raia wa China anasema kuanza tena safari za reli za mwendo kasi kumerahisha harakati zao na kuwasogeza zaidi nyumbani kwao .

Kwa takriban miaka miatu wakati wa janga, haikuwa rahisi kwa China kwa njia yoyote kutembea na kuendelea na shughuli za kawaida, aliongeza kusema Mang.

XS
SM
MD
LG